
MKUTANO WA MAJADILIANO YA KISEKTA
-
Posted on May 29, 2023 10:36
TCCIA na TNBC kwa kushirikiana na Wizara ya Madini, iliandaa Mkutano wa
Majadiliano ya Kisekta (Ministerial Public Private Dialogue - MPPD) kwa ajili ya
kujadili changamoto na Fursa zilizopo katika Sekta ya Madini na kupendekeza
mikakati itakayowezesha sekta husika kuchochea biashara na uwekezaji nchini.
Mkutano huo uliongozwa na Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Doto M. Biteko (Mb), ambapo sekta zinazo husiana na Madini zilihudhuria na kushiriki moja kwa moja katika ukumbi wa Mikutano Makumbusho ya Taifa Dar esSalaam leo tarehe 13 Februari, 2023 katika Ukumbi wa Madini, Dar Es
Salaam.